Home » » Wakulima watataelimu ya kuboresha mazao, kilimo mikoa mitatu ya nyanda za ju kusini

Wakulima watataelimu ya kuboresha mazao, kilimo mikoa mitatu ya nyanda za ju kusini

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Abiud Gamba mmoja wa menejimenti ya ACTN
 Mkurugenzi wa ACTN Said Komwa


Washiriki wa mafunzo ya kuboresha kilimo mikoa mitatu ya 
Njombe, Ruvuma na Iringa

WAKULIMA kutoka katika vikundi mbalimbali kutoka halamashauri za Namtumbo wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma, Ludewa Mkoani Njombe na halmashauri ya Mufindi Mkoani Iringa wametakiwa kuhakikisha wanahifadhi vizuri mazao yao ili kuingiza katika ushindani wa soko la mazao yao na kuhakikisha wanasafisha na kukausha vizuri.

Wito huo umetolewa na Frank Mhando kutoka kampuni ya Agra inayojishughurisha na kuwasaidia wakulima kuinuka kiuchumi, kwa kuboresha mazao yao kutoka kilimo hadi mavuno wakati wa semina kwa wakulima hao iliyoandaliwa Taasisi ya African Conservation Tillage Network, (ACTN) na kufanyika Njombe mjini.

Alisema kuwa wakulima wengi wamekuwa wakilalamika masoko hamna kitu kinacho shusha bei ya mazao ni kutokana na kuto kuwapo kwa utunzaji bora wa mazao na kushindwa kuyaweka katika hali ya usafi.

Mhando alisema kuwa wakulima wengi wamekluwa wakaweka mazao yao katika hali ya uchafu kitu kinacho wakimbiza wanunuzo na kuleta malalamini ya kuto nunuliwa kwa mazao hayo.

Alisema kuwa; “Wakulima wamekuwa walikusanya mahidi yaliyo vunjika vunjika na mazuri kitu kinacho kimbiza wateja kwani nao wakinunua kwako watashindwa kuuza kwa kuwa sio masafi, lakini kama utaweka katika hali ya usafi utaweza kupoata wateja kwa bei nzuri.

Aidha kwa upande wao wakulima kutoka Songea, Namtumbo, Ludewa na Mafinga wamesema kuwa kwa kupata elimu hiyo waliyo itata wataendeleza kilimo chao kwa kwenda kufuiata kanuni za uhifadhi, usafi wa mazao, na kulima kilimo hifadhi ili mashamba yao kuwa imara na kurutubika.

Wamesema kupitia elimu hiyo wataenda kuielimisha na jamii inayo wazunguka ili nako kujitahidi kulima kilimo hifadhi na kuweka safi mazao yao kwa kuhufadhi bira kuweka viwatilifu vya maji ili kuwa na mazao yenye usalama.

Akifunga mkutano huo Mkurugenzi wa ACTN, Said Komwa alisema kuwa wakulima wajitahitu kulima kilimo hifadhi kwaajili ya kujipatia kipato maradufu ya wanavyo pata sasa na kuwa kilimo hifadhi hulinda shamba na kusisitiza kuchambua mazao yao ili mnunuzi asipate mashaka na mazao yao.
Alisema kuwa wakulina wanawajibu wa kuhufadhi kwa pamoja mazao yao ili kupata wateja wa jumla kuliko kuuza mazao mmoja mmoja na hatimaye kufikia malengo yao ya kuwa na maisha bora.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa