Home » » `JAMII FICHUENI MTANDAO WA UFADHILI MAUAJI ALBINO`

`JAMII FICHUENI MTANDAO WA UFADHILI MAUAJI ALBINO`

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi
 
Maaskofu na mamia ya wanawake kutoka mikoa mbalimbali nchini wanaohudhuria kongamano la maombi katika mji mdogo wa Makambako mkoani Njombe, wameitaka jamii nchini kusaidia kuufichua   mtandao wa wafanyabiashara wanaofadhili wauaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).
Kauli ya Maaskofu na wanamaombi hao imekuja siku mbili tangu Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi, kuelezea masikitiko yake juu ya vitendo viovu wanaofanyiwa watu wenye ulemavu wa ngozi.

Baadhi ya mikoa waliyotoka maaskofu na wanamaombi hao ni ya Mbeya, Iringa, Mwanza, Shinyanga, Tanga, Kilimanjaro, Mara, Arusha, Morogoro, Ruvuma, Dodoma na Rukwa.

Maaskofu na wanawake hao, wamewalaani wauaji na watu wanaoufadhili mtandao huo wakisema   wanajulikana kwani wanaishi hapa nchini.

"Sisi tunaamini kama viongozi wa serikali watasimamia kikamilifu kukabiliana na unyama huu wa mauaji ya albino, itashinda," ilisema sehemu ya tamko lao lililosomwa na Askofu Msaidizi wa Kanisa la Kiinjili la Kipentekoste nchini, Mchungaji William Mwamalanga.

Aidha, wamemuomba Rais Jakaya Kikwete, kutangaza mauaji ya albino janga la kitaifa.
 
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa