VIONGOZI NA WATAALAM WA OFISI YA RAIS, TUME YA MIPANGO WAKAGUA MAENDELEO MRADI WA MAKAA YA MAWE MCHUCHUMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais Tume ya Mipango, Dkt. Philip Mpango (wa pili kulia), akipata maelezo juu ya Mradi wa Makaa ya Mawe Mchuchuma kutoka kwa Meneja Utawala Msaidizi wa kampuni ya Tanzania – China International Mineral Resources Limited (TCIMRL) Bw. Israel Mkojera. Pamoja nae ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NDC Bw. Mlingi E. Mkucha (wa kwanza kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Viwanda Mama wa NDC Bw. Ramson Mwilangali (wa kwanza kushoto), Naibu Katibu Mtendaji, Tume ya Mipango Bi. Florence Mwanri (wa pili kushoto), Erasmus Masumbuko, Tume ya Mipango (wa tatu Kushoto).
 Viongozi pamoja na Maofisa kutoka Tume ya Mipango wakiangalia sehemu ambayo makaa ya mawe yanaonekana juu ya ardhi. Kulia ni mhandisi wa madini kutoka kampuni ya TCIMRL. Kampuni hii ni ya ubia kati ya Serikali ya Tanzania, na kampuni ya Sichuang Hongda Group Limited ya China. 
 Sehemu ambayo makaa ya mawe yanaoneka kwa juu katika uhalisia wake.
Shimo hili lilichimbwa mwaka 1956 kwa ajili ya utafiti kuangalia tabaka za makaa ya mawe katika eneo hilo la Mchuchuma.

HABARI NJEMA KWA WALE WOTE WALIOKOSA NAFASI KUENDELEA NA MASOMO KIDATO CHA TANO SERIKALINI , SASA MNAWEZA KUOMBA KUSOMESHWA SOMA HAPA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


WAANDISHI WA HABARI WA MKOA WA NJOMBE WAKABIDHIWA VYETI VYA USHIRIKI WA MAFUNZO YALIYOTOLEWA NA MCT‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Katibu wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe Hamis Kassapa akipokea cheti cha kushiriki mafunzo yaliyotolewa na baraza la habari Tanzania MCT kwa waandishi wa habari wa mkoa huo jana Juni 19, 2014
Mtangazaji wa Uplands Fm Zenobia Mtei akipokea cheti chake kutoka kwa wawakilishi wa MCT
David Jothamson kutoka Kings FM ya Njombe akipokea cheti chake cha kushiriki mafunzo
Mtangazaji Veronica Mtauka wa redio Kitulo FM ya wilayani Makete mkoani Njombe akipokea kwa furaha cheti chake kama mshiriki wa mafunzo hayo
Mkurugenzi wa Ice FM ya Makambako mkoani Njombe MCDonald Mase akipokea cheti chake
 Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe Mercy James akikabidhiwa cheti chake
 Meneja wa kitucha redio Uplands Fm, Novatus Lyaruu akipokea cheti chake kama mshiriki wa mafunzo hayo
Mwandishi wa habari wa gazeti la Majira na mtandao wa Habari Ludewa Blog NIckson Mahundi akikabidhiwa cheti chake
Mtangazaji wa Best FM ya Ludewa mkoani Njombe akipewa cheti chake cha ushiriki wa mafunzo hayo
Mmiliki wa Eddy Blog Edwin Moshi akipokea cheti cha mafunzo hayo ya siku nne yaliyoandaliwa na MCT.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na baraza la habari Tanzania (MCT) kwa kushirikiana na chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe (NPC) yenye lengo la kuwasaidia waandishi hao kuandika habari kwa kufuata weledi wa taaluma hiyoPICHA ZOTE NA EDWIN MOSHI
 

MKUU WA WILAYA YA MAKETE ATOA RAI KWA JAMII YA MAKETE KUSAIDIA WATOTO YATIMA NA WAISHIO KWENYE MAZINGIRA HATARISHI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mkuu wa wilaya ya Makete mwenye suti nyeusi (aliyesuka nywele) Mh. Josephine Matiro, mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu Helen Kijo Bisimba (kulia kwa mkuu wa wilaya) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto walioshiriki maadhimisho hayo.
 Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro(wa tatu kushoto walioketi) na Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu Helen Kijo Bisimba (wa pili walioketi kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa shirika la wasaidizi wa kisheria Makete
 Katika picha ya pamoja na wanafunzi wa sekondari ya Iwawa Makete ambao nao walishiriki
 Wanafunzi wa shule ya msingi Ndulamo wakiwa katika picha ya pamoja.(Picha/habari na Edwin Moshi na Conrad Mpila, Makete.)
Imeelezwa kuwa ni jukumu la kila mmoja kuwasaidia watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi, na si kuiachia serikali ama mashirika yasiyo ya kiserikali peke yao kufanya kazi hiyo
 
Kauli hiyo imetolewa leo hii Juni 16 na mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kitaifa (kwa asasi zisizo za kiserikali) katika viwanja vya mabehewani kata ya Iwawa wilayani Makete mkoani Njombe

Hata hivyo mkuu wa wilaya hiyo amekiri kuwepo kwa changamoto ya watoto walio wengi Wilayani Makete ambao ni Yatima na waishio katika mazingira magumu ambao wanahitaji msaada wa kila mmoja

"Ni kweli wilaya ya Makete ina watoto ambao ni yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi, wengine wanalelewa katika vituo maalum vilivyopo wilayani mwetu, hivyo ni jukumu letu kuwasaidia kila mtu kwa kadri ya uwezo wake, mwenye sabuni, kalamu, fedha ama chochote anaweza kufanya hivyo kwa wakati wake" amesema Matiro

Katika risala iliyosomwa na mwanafunzi Gaudencia Malangalila wa Shule ya msingi Ndulamo kwa niaba ya wanafunzi wenzake amesema Kuwa watoto walio wengi wanakabiliwa na unyanyasaji kwa kufanyishwa Kazi ngumu na hatarishi,kutopata haki katika huduma za matibabu,walezi kunyang'anya misaada wanayopewa na wadau mbalimbali

Naye Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) Bi. Helen Kijo Bisimba amesema Kuwa kwa Tafiti alizofanya amebaini Kuwa kuna watoto ambao waliondoka kwenda nje ya Makete kwa kufanya Kazi na hawarudi tena huku wazazi hawajui Kama wapo hai au la,kwani hata mawasiliano na wazazi ama walezi wao bado ni magumu

Hivyo amewasihi wazazi/walezi Kuwa makini na watoto wao pindi wanapoitwa kwenda kufanya Kazi maeneo ya mbali kwani mara nyingi huko wanakokwenda wanakutana na mambo ambayo ni kinyume na walioyatarajia

Katika maadhimisho hayo kikundi cha wazazi kutoka Kijiji cha Isapulano na Ndulamo Maarufu Kama mama mkubwa wamesema Kuwa vikundi hivyo vitaendelea Kulinda haki za watoto na kutoa ujumbe kwa jamii kwa njia ya sanaa  na kufanya uchunguzi dhidi ya watoto wanaofanyiwa unyanyasaji na watatoa taarifa katika ngazi husika na wakigundulikaa wahusika wachukuliwe hatua za kisheria
 
Kauli mbiu ya mwaka huu ni "kila mtoto ana haki ya elimu bora bila vikwazo"

CWT,TGNP,WATAKA BAJETI KUZINGATIA MAENEO MUHIMU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais wa CWT, Gratian Mukoba
Chama cha Walimu  nchini (CWT) kimesema wananchi wanahitaji bajeti itakayowapatia mahitaji muhimu kama elimu, afya, maji na ulinzi.
Rais wa CWT, Gratian Mukoba (pichani) , alisema bajeti ya elimu inatakiwa kuwa asilimia sita ya pato la taifa, lakini hadi sasa bajeti inayotengwa na serikali ni asilimia moja.

Mukoba alisema bajeti nzuri ni ile ambayo inampatia mwananchi mahitaji ya vitu muhimu ambavyo wananchi wanatarajia kuvipata.

“Vitu kama elimu, afya, maji na ulinzi ni muhimu, watu wanahitaji, afya bora ili waweze kufanya kazi na kupata kipato, ulinzi ni muhimu kwani kuna makundi yameibuka kama ‘Panya wa Rwanda’ na ‘Mbwa mwitu’ ambayo yanahatarisha usalama wa wananchi, hivyo wananchi wanahitaji kusikia ulinzi unaimarishwa,” alisema Mukoba.

Alisema ili taifa hili liweze kuendelea na kukuza uchumi wake ni vyema serikali ikazingatia vipaumbele hivyo ili kuendelea  kuinua uchumi wa wananchi wake.

Nao Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), umesema   kama bajeti itakayosomwa leo haitazingatia  na kuweka vipaumbele muhimu kama afya na maji bado haitamsaidia mwananchi wa kawaida.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi, alisema katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), Wizara ya Afya haijahusishwa, suala ambalo ni hatari kwani jamii inahitaji kuwa na afya bora ili kufanya shughuli za maendeleo.

“Bajeti ya serikali bado haijaweza kumnufaisha mwananchi wa kawaida kama vile ambavyo wananchi wanatarajia, mfano masuala muhimu kama afya na maji ni miongozi mwa mambo ambayo bado yanawaumiza wanawake na vijana walioko pembezoni,” alisema Liundi.

Alisema kipaumbele cha sekta binafsi ambayo serikali imeboresha na kukuza uchumi wa nchi bado hakijaweza kumnufaisha mwananchi wa kawaida.

Alifafanua kuwa ukuaji wa uchumi bado haujawafikia au kuwanufaisha wananchi ambao wako pembezoni hasa wanawake na watoto.

Alisema kwa upande wa sekta ya usafirishaji bado pia haijaweza kuwanufaisha wananchi wa kawaida ambao ni wakulima wa mazao mbalimbali ambao wanatarajia kutumia barabara ili kusafirisha mazao yao.

CHANZO: NIPASHE

MKUU WA WILAYA YA MAKETE AFUNGA RASMI MAFUNZO YA MADEREVA BODABODA NA WAJASIRIAMALI MAKETE‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro akitoa hotuba yake wakati akifunga mafunzo kwa madereva bodaboda wilayani Makete. Mafunzo hayo yametolewa na shirika la APEC
 Madereva bodaboda wakifurahia kupatiwa vyeti vya mafunzo hayo.
 Bi Rehebian Mahenge ambaye alikuwa katibu katika mafunzo hayo akisoma risala mbele ya mgeni rasmi
 Bi Mahenge akimkabidhi risala mkuu wa wilaya ya Makete Mh Josephine Matiro ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika mafunzo hayo
Mkuu wa polisi wilaya ya Makete Alfred Kasonde akitoa nasaha kwa wahitimu wa mafunzo hayo
 Mkuu wa wilaya akitoa hotuba yake
 Mkurugenzi wa APEC Bw. RespiciusTimanywa akitoa maelezo ya awali jinsi walivyoendesha mafunzo hayo na matarajio wanayoyategemea kutoka kwa wahitimu hao

 Miongoni mwa wahitimu wa mafunzo hayo ambaye pia ni askari polisi wilayaani Makete Afande Moses akipokea cheti chake
 Picha ya pamoja na mgeni rasmi
 Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Josephine Matiro akiteta jambo na Mkurugenzi wa APEC Bw. Respicius Timanywa mara baada ya kumaliza kufunga rasmi mafunzo hayo
 Baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Makete wakiwa kwenye picha ya pamoja
 wawezeshaji wa mafunzo hayo wakiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalam wilaya ya Makete

WASHANGAZWA NA USHINDI WA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE USAFI WA MAZINGIRA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na James Festo, Njombe.

KATIKA kuelekea siku ya maadhisho ya mazingira  ambayo hufanyika june tano ya kila mwaka  huku Halmashauri ya mji wa Njombe ikiwa inaendelea kushika nafasi za juu kwa usafi   wananchi wake wameendelea kuitupia lawama za kushindwa kuzoa takataka  kwenye vizimba hali ambayo inaweza kusababisha  magonjwa ya mlipuko.

Hali hiyo inakuja kufuatia kusuasua kwa uzoaji taka  katika vizimba vya takataka vikiwemo vilivyopo karibu na maeneo yanayotumika katika uuzaji wa vyakula  kitu ambacho kinaweza kusabisha madhara makubwa kwa wauzaji pamoja na wateja wao

Mwandishi wa habari hii alitembelea na kujionea  vituo mbalimbali Ndani ya halmashauri ya Mji wa Njombe  hali mbaya ya takataka zilizofurika  nje ya vizimba  licha ya wananchi kuendelea na biashara  likiwemo eneo nyuma ya kituo cha mabasi mjini njombe.

Wakizungumza na majira baadhi ya wafanyabiashara hao walisema kuwa tangu kusimama  kwa mawakala waliokuwa wakifanya kazi hiyo ya kuzoa takataka kwenye vizimba na Halmashuri kuvaa jukumu hilo  mwenendo umekuwa wa kusuasua na kueleza kushangazwa  kuona wakilipa ushuru kila uchao wakati taka hazizolewi kwa wakati.

 "   sasa hivi michango imesitishwa  ndio maana ya kwenye vizimba taka ni nyingi.... labda kila mwananchi awe anachangia  kila kaya ...tunataka tuchangie..... tukisema tufanye hivi hatufiki ...... wakala ameshindwa kufanya kazi kwa sababu  kipato anachopata halmashauri  ni kidogo "   walisema wafanyabiashara hao.

Aidha Wafanyabiashara  hao waliiomba halmashuri kutumia  fedha zinazokusanywa katika ushuru wa soko kutumika katika kufanya usafi wa soko hilo na kuwasisitiza watumishi wa sekta hiyo kuacha uzembe wa kukaa ofisini.

Andove Mgani ni mwenyekiti wa  soko la  wafanyabishara lililopo nyuma ya kituo cha mabasi cha Njombe alisema kuwa tangu Halmashuri ya Mji ianze kusimamia yenyewe  zoezi ya utoaji wa taka hizo imekuwa ikizidiwa na kusababisha  taka kukaa zaidi ya wiki  kitu ambacho ni hatari kwa wananchi  mjini hapa.

"  ninachojua zamani taka taka na yule wakala alikuwa makini na kazi yake lakini baada ya kusimamiwa na halmashauri  vizimba vya hapa mjini vyote vinakaa na takataka muda wote  kama wafanyabiashara tungekuwa na uwezo wa kuamua  tungemuaomba arudi afanye kazi ya kuzoa takataka"   alisema Bw Ndonya.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Bw. Venance Msungu alikiri kuwepo kwa tatizo hilo la uzoaji wa takataka  alisimama kutokana kiasi cha fedha aliyokuwa akilipwa huku mji wa Njombe ukiendeea kuongezeka kwa uchafu.

Alisema kuwa katika kipindi cha miezi miwili baada ya wakala huyo Halmashauri hiyo imekuwa ikiendelea na zoezi hilo  huku wakisubiri mwezi julai mwaka huu wa kutangazwa kwa mzabuni ambaye ataanza kufanya kazi hiyo ambaye atakuwa na vifaa vya kutosha tofauti na Halmashauri  ambayo imekuwa ikitumia magari mawili pekee.

"  hata waandishi wa habari inayostahili watu wanaongea kwamba uchafu bado tatizo jambo linaonyesha kukosa uelewa wa kulinganisha na sehemu zingine  hapa nchini....zabuni zitafunguliwa mwezi huu  wa sita  na inapoanza mwezi julai  tutakuwa na mzabini mwenye vifaa vya kutosha vya kutolea uchafu"   alisema bw Msungu.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa