Home » » WAFANYABIASHARA WALALAMIKIA UCHAKAVU WA SOKO KUU MAKAMBAKO

WAFANYABIASHARA WALALAMIKIA UCHAKAVU WA SOKO KUU MAKAMBAKO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAFANYABIASHARA katika soko kuu la Makambako mkoani Njombe wameilalamikia Halmashauri ya Mji kushindwa kukarabati soko hilo  kwa muda mrefu.

Uchakavu huo umedaiwa  unasababisha bidhaa ambazo zinahifadhiwa ndani yake kuharibika hususani kipindi hiki cha Mvua.

Wafanyabishara hao wamesema, hali ya soko kwa sasa ni mbaya na usalama wa mali zao umekuwa  wa mashaka licha ya kwamba ushuru umekuwa ukitolewa hata hivyo maombi yao ya kufanyika ukarabati hayajasikilizwa na uongozi.

Mrundikano wa taka katika dampo  pia umekuwa kero na kuhatarisa usalama wa afya zao,hali inayotokana na kuchelewa kuzizoa taka hizo.

Mkurugenzi wa Halamashauri ya Mji Makambako Tina Sekambo amesema  kuwa katika bajeti ya mwaka 2014/15 jumla ya  sh, Milioni 150 zimetengwa kwaajili ya ukarabati wa soko hilo.
 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa