MKUTANO MKUU WA TATU WA PSPF WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais mstaafu wa awamu ya pili,Alhaj Ali Hassan Mwinyi, akizindua huduma mpya ya PSPF Pamoja nawe na PSPF call centre, itolewayo na mfuko wa Pensheni wa PSPF, baada ya kufungua Mkutano mkuu wa tatu wa wadau wa mfuko huo Feb 26.2014.
 Mgeni rasmi Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Hassan Mwinyi, kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, kulia kwake ni Ndugu Peter Ilomo aliyemwakilisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSPF George Yembesi, Mkurugenzi Mkuu PSPF, Adam Mayingu na Katibu Mkuu MPAIC, John Haule
Wakurugenzi wa idara mbalimbali za mfuko wa Pensheni wa PSPF, mstariu wa mbele, wakiwa miongoni mwa wajumbe wanaohudhuria mkutano mkuu wa tatu wa wadau wa mfuko huo kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa julius Nyerere jijini Dar es Salaam Februari 26, 2014.

  Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSPF, Neema Muro akijadili jambo na mmoja wa wadau wa PSPF

Usikivu 
 Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima akimkaribisha Mgeni Rasmi Rais Mstaafu wa Awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi alipowasili kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimtaifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana, kuhudhuria mkutano mkuu wa tatu wa Mfuko wa PSPF wa wadau Februari 26.2014.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu (kushoto), akimkaribisha Mgeni Rasmi Rais wa Mstaafu Ally Hassan Mwinyi kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimtaifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, kuhudhuria mkutano mkuu wa tatu wa Mfuko wa PSPF wa wadau Februari 26.2014.


 Kutoka kushoto ni Meneja wa Kitengo Mawasiliano ya simu, Fatma Elhadgy, Meneja wa Mawasiliano, Masoko na Uenezi wa PSPF, Costantina Martin na Ephraim Kibonde 

 Mgeni rasmi Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Hassan Mwinyi 
Mgeni rasmi Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ally Hassan Mwinyi akionyesha zawadi aliyopewa na PSPF, kushoto kwake ni Ndugu Peter Ilomo aliyemwakilisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSPF George

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA WADAU WA PSPF

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MFUKO WA PENSHENI WA
PSPF

TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA WADAU
Mfuko wa Pensheni wa  PSPF unatangaza kwamba kutakuwa na Mkutano Mkuu wa tatu wa wadau utakaofanyika tarehe 26 na 27  Februari 2014 kuanzia saa mbili na nusu asubuhi hadi saa kumi jioni katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo barabara ya Shaban Robert  jijini Dar es salaam.
Madhumuni ya Mkutano huu ni kutoa taarifa ya hesabu ya mwaka na utendaji wa Mfuko na kutathmini mafanikio na changamoto zinazokabili Mfuko na sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa ujumla.
“PSPF - TULIZO LA WASTAAFU”
Mkurugenzi Mkuu
Mfuko wa Pensheni wa PSPF,
Makao Makuu,Golden Jubilee Towers,  S.L.P 4843. Dar-es-Salaam.
Simu: +255222120912/52 au +255222127375 /6
 Nukushi: +255222120930

 Barua pepe:pspf@pspf.tz.org

NANI WAMEIBA SH.480 BILIONI HAZINA

Tangu gazeti dada la The Citizen lichapishe mwishoni mwa wiki habari za upotevu wa Sh480 bilioni katika Wizara ya Fedha, Serikali imekaa kimya kama vile wizi huo ni tukio la kawaida, hivyo halihitaji maelezo ya kina wala ya haraka. Wananchi walitegemea kwamba Serikali ingetoa kauli haraka iwezekanavyo kuhusu mazingira ya upotevu huo na hatua inazochukua kuwawajibisha wahusika.
Tunasema kiasi hicho cha fedha zilizoibwa ni kikubwa kwa sababu ni zaidi ya bajeti ya mwaka kwa baadhi ya wizara, zikiwamo wizara kubwa kama ya Uchukuzi ambayo katika mwaka wa fedha wa 2013/14, kwa mfano ilitengewa Sh491 bilioni.
Tunaambiwa Sh480 bilioni zilizopotea katika Wizara ya Fedha zinaweza kujenga kilomita 375 za barabara kwa kiwango cha lami ikiwa ni urefu wa kutoka Dar es Salaam hadi Gairo, kilomita chache kutoka Dodoma. Tujiulize kiasi hicho cha fedha kingeweza kugharamia madawati, zahanati na madarasa mangapi kwa ajili ya wagonjwa na wanafunzi wetu.
Pamoja na ukimya wa Serikali kuhusu wizi huo, tumetiwa moyo na hatua ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Fedha za Serikali (PAC), ambayo imemtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG), Ludovick Utouh kuchunguza upotevu huo wa kiasi hicho kikubwa cha fedha ambacho kilitumika pasipo maelezo katika kipindi cha miaka miwili ya fedha cha 2012/13 na 2013/14.
Wasiwasi wa kamati hiyo ni kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kuwapo kwa mtandao mkubwa wa wizi wa fedha za Serikali katika Wizara ya Fedha. Jambo hilo limethibitishwa na vitendo vya wizi wa kimtandao ambavyo vimekuwa vikifanywa na baadhi ya watumishi wake wakishirikiana na baadhi ya watendaji wa Tamisemi.
Ugumu uliopo hapa ni kwamba haijulikani kama fedha hizo zilizopotea zilitokana na kodi za wananchi au wafadhili ambao walichangia Sh842 bilioni katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2012/13. Ni sahihi kabisa kwa Kamati hiyo ya Bunge kushangazwa na kuendelea kuwapo kwa vitendo vya ufisadi serikalini, hasa kwa kuzingatia ukweli kwamba ripoti za CAG kila mwaka zimekuwa zikifichua wizi wa mabilioni ya fedha katika Serikali Kuu na Serikali za Mitaa. Kujirudia kwa vitendo hivyo kila mwaka ni ishara kwamba Serikali haina dhamira ya kupambana na vitendo hivyo.
Mwenendo huo wa Serikali unashangaza, hasa kutokana na ukweli kwamba mwaka 2013/14 ilikuwa na nakisi ya Sh847 bilioni katika bajeti yake. Hivyo, utekelezaji wa mipango yake ya maendeleo ingekwama kama siyo kukopa mabilioni ya fedha kutoka vyanzo vya nje na ndani ya nchi.
Matokeo yake ni kuzidi kuongeza mzigo wa Deni la Taifa ambalo limefikia Sh27 trilioni sasa, huku ikishindwa kukusanya kodi na kupanua wigo wa vyanzo vya kodi. Ndiyo maana iko hoi kifedha na karibu shughuli zake zote zimesimama, huku ikisuasua kulipa mishahara ya watumishi wake.
Pamoja na hali hiyo mbaya kifedha, bado vitendo vya wizi na ufisadi serikalini vinaendelea kama tunavyoshuhudia vikishamiri katika Wizara ya Fedha. Ni jukumu la Serikali kudhibiti ubadhirifu na ufisadi miongoni mwa watumishi wake, vinginevyo uchumi wetu utazidi kudidimia. Kwa kuanzia iwasake na kuwawajibisha wote walioiba Sh480 bilioni kutoka Hazina.
Chanzo;Mwananchi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MKUU WA WILAYA YA NJOMBE ATEMBELEA SHULE YA MAKETE GIRLS


 Mkuu wa mkoa wa Njombe kapteni Mstaafu Aseri Msangi(katikati) akikagua majengo ya shule mpya wa wasichana wilayani Makete, kushoto ni mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro na kulia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Daniel Okoka.
 Ukaguzi huo ukiendelea.
 Wananchi wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni Msangi(hayupo pichani) akizungumza nao
 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akizungumza kwenye mkutano shuleni hapo
 Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi akizungumza na wananchi shuleni hapo.
========  ======  =======
Habari/picha na  Edwin Moshi, Makete.

Kufuatia kukamilika kwa kiasi kikubwa majengo ya shule mpya ya sekondari ya wasichana Makete iliyojengwa katika kijiji cha Utweve kata ya Ukwama wilayani Makete, mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni mstaafu Asseri Msangi ameagiza shule hiyo iandikishwe ili ianze kutumika.
Mkuu wa mkoa ametoa agizo hilo hii leo Februari 11, 2014 wakati wa ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya elimu wilayani Makete, ambapo baada ya kufika shuleni hapo ameridhishwa na ujenzi wa shule hiyo na kuona haina sababu ya shule hiyo kuendelea kukaa bila kuandikishwa ili ianze kupokea wanafunzi.
Akizungumza na wananchi wa vijiji viwili vinavyojenga shule hiyo ambavyo ni Utweve na Masisiwe, mkuu huyo wa mkoa mbali ya kupokea na kutjibu kero za wananchi, amekasirishwa na tabia ya wazazi wa vijiji hivyo kuwaambia watoto wao wafeli kwa makusudi ili wasiendelee na masomo ya sekondari.
"Ndugu zangu dunia tuliyopo sasahivi, si ile tuliyoishi zamani, mtoto asiposoma ni matatizo kwake, na ninyi wazazi wenye tabia ya kuwaambia watoto wenu wafeli kwa makusudi mnatupelekea taifa letu kaburini na sisi hatutakubali, tunaomba muiache hiyo tabia, somesheni watoto wenu" alisema Msangi.
Katika hatua nyingine Kapteni Msangi amechangia kiasi cha shilingi milioni 1 kwa ajili ya shule hiyo maalum kwa ajili ya wasichana kama njia mojawapo ya kusaidia ujenzi wa shule hiyo ambayo inatarajiwa kuanza hivi karibuni.
Shule hiyo pekee ya wasichana wilayani Makete inajengwa na serikali kwa kushirikiana na wazawa wa Makete wanaoishi nje ya wilaya hiyo, wananchi pamoja na wadau mbalimbali.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MVUA KUBWA ZINAZO ENDELEA KUNYESHA: MKUU WA MKOA WA NJOMBE AKWAMA KUTOKANA NA TOPE.


Gari la mkuu wa mkoa wa Njombe likiwa limekwama kwenye tope kijiji cha utweve makete. 
 Wadau wakisukuma gari hilo, na huyu ni mwenyekiti wa kijiji cha Utweve akijitahidi kusukuma.
 Hali tete hapa, gari hilo likiwa limenasa mtaroni
 wadau wakijitahidi kuvuta gari hilo
 jitihada zikiendelea.
Gari la mkuu wa mkoa wa Njombe, kapteni mstaafu Aseri Msangi limekwama kwa zaidi ya saa kadhaa katika kijiji cha Utweve wilayani Makete wakati akiwa ziarani kukagua maendeleo ya sekondari ya wasichana makete inayojengwa kijijini hapo

Adha hiyo ilimkumba mkuu wa mkoa baada ya mvua kubwa kunyesha wakati akifanya mkutano na wananchi shuleni hapo mara baada ya kuikagua shule hiyo na kuridhishwa na jinsi ilivyojengwa

Mtandao huu wa eddy blog umeshuhudia magari mengine yaliyokuwa yametangulia gari la mkuu wa mkoa yakipita eneo hilo lililokuwa na utelezi mwingi huku gari hilo la mkuu wa mkoa likikwama kutokana na utelezi huo

Jitihada za kulinasua gari hilo zilifanywa na msafara mzima ulioambatana na mkuu wa mkoa pamoja na wananchi wa kijiji hicho ambapo zoezi hilo lilichukua zaidi ya saa moja kutokana na mvua kuzidi kunyesha zaidi

Jitihada hizo zilizaa matunda na hatimaye gari hilo lilinasuliwa na mkuu wa mkoa kuendelea na safari yake, na hakuna madhara yoyote yaliyotokea

HABARI/PICHA NA EDDY BLOG
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Serikali yaanza kusaka masoko ya mazao

SERIKALI mkoani Njombe kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara imeanza kutafuta ufumbuzi tatizo la ukosefu wa masoko ya uhakika kwa mazao ya kilimo ikiwemo viazi mviringo ambapo, ujenzi wa soko la kimataifa mjini Makambako utasaidia kumaliza tatizo hilo.
Akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015 kwa kipindi cha miezi nane iliyopita, Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Assery Msangi, alisema katika kipindi hicho pamoja na mafanikio yaliyopatikana mkoani hapa, bado kumekuwa na changamoto mbalimbali.
Alitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na baadhi ya wakulima kukataa kutumia mbolea ya minjingu kwa madai ya kuwa haina ubora katika kilimo. Aliongeza kuwa, serikali inaendelea kuwahamasisha wakulima kuimarisha vyama vya ushirika wa mazao ili kuwa na nguvu ya pamoja wakati wa kupanga ili kuuza mazao kwa bei nzuri.
Alisema, kwa sasa mkoa unaendelea kuiomba wizara ya kilimo kutoa nafasi kwa mkulima kuchagua ni aina gani ya mbolea anayotaka kutumia badala ya kuendelea kuwalazimisha kutumia minjingu ambayo wakulima wengi wameonesha kutokuwa na imani nayo.
"Tunaendelea kuhamasisha wananchi na tunaiomba wizara kama inawezeka na msimu ujao watoe uhuru mtu achague aina ya mbolea ambayo anataka kutumia," alisema Msangi.
Aliongeza kuwa, mwaka ujao wa fedha serikali imekusudia kupunguza changamoto za miundombinu ikiwemo kuboresha barabara zitakazoweza kuunganisha kati ya wilaya moja hadi nyingine bila matatizo ikiwemo wilaya za Ludewa na Makete.

Mwananchi

NAIBU WAZIRI WA MAENDELO YA JAMII PINDI CHANA APOKELEWA KWA KISHINDO WILAYANI RUDEWA.


 
 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,Pindi Chana akimkaribisha Mama yake mzazi Regina Mlowe kuzungumza machache katika sherehe za kumkaribisha zilizofanyika katika ukumbi wa CCM wilaya ya Rudewa
 Mama mzazi akiwashukuru wananchi wa Rudewa katika sherehe za kumkaribisha Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,Pindi Chana.
 baadhi ya wanachama wa CCM wakiwa katika sherehe za kumkaribisha Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,Pindi Chana.
 Mkuu wa Wilaya ya Rudewa Juma Solomon Madaha akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,Pindi Chana.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,Pindi Chana akicheza muziki na baadhi ya viongozi wa ccm wilaya ya Rudewa

(Picha zote na Denis Mlowe).
Michuzi Media Group

MKUU WA WILAYA YA MAKETE AWAKUTANISHA POLISI NA MADEREVA WA BODABODA



 Kikao cha waendesha bodaboda kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete hii leo.
Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro akionesha kitabu cha polisi kwa ajili ya kutoza faini za makosa ya usalama barabarani.
Mkuu wa polisi(OCD) wilaya ya Makete Alfred Kasonde akionesha risiti za faini ambazo zimetelekezwa na baadhi ya madereva ambao wengi wao wamekuwa wakilalamika kuwa fedha hizo zimeliwa na askari.
 Meneja Msaidizi wa TRA Makete Hamis Zumba akifafanua jambo kwa madereva bodaboda Makete.
 Dereva bodaboda aliyejitambulisha kama Alex akiuliza swali kwenye kikao hicho
 Mwalimu wa VETA Makete Bw. Mathew Komba akifafanua jambo kwenye kikao hicho

Na Edwin Moshi, Makete
Kutokana na ukosefu wa elimu ya sheria barabarani miongoni mwa madereva bodaboda wilayani Makete mkoani Njombe kunakopelekea madereva hao kukamatwa na askari wa usalama barabarani mara kwa mara, mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro amefanya kikao na waendesha bodaboda hao

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete, waendesha bodaboda hao walipata fursa ya kutoa kero zao na kuuliza maswali ambayo yalikuwa yakijibiwa papo kwa papo na Muu wa polisi wilaya ya Makete, askari wa usalama barabarani na Meneja msaidizi wa TRA Makete

Akizungumza kwenye kikao hicho Mkuu wa polisi wilaya ya Makete (OCD) Alfred Kasonde amekanusha vikali tuhuma zinazoelekezwa kwa askari wake kuwa wanakula fedha wanazotoza kama faini kwa vyombo vya usafiri wanavyotoza kutokana na makosa mbalimbali na kuongeza kuwa ni vingumu kwa askari ambaye amekuandikia faini ya kosa lako kwenye kitabu cha serikali kula fedha hiyo

Bw. Kasonde amesema askari wake hawana vitabu vya risiti na hawaruhusiwi kutembea navyo kwa kuwa jeshi la polisi lina wahasibu wanaokusanya fedha hizo, hivyo kwa wilaya ya Makete dereva akiandikiwa faini na askari, askari haruhusiwi kupokea fedha na badala yake atakuandikia karatasi maalum maarufu kama notification na baada ya hapo dereva huyo atakwenda kulipa faini hiyo kituoni

Amewataka madereva hao kuacha kuwapa fedha ya faini askari hao na badala yake wahakikishe askari aliyewakamata anaandika kosa hilo kwenye kitabu cha faini, huku akionesha rundo la risiti za madereva bodaboda ambao wamelipia faini lakini hawajafika kuchukua risiti zao kwa madai kuwa fedha walizotoa zililiwa na askari

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Makete mh. Josephine Matiro amewataka madereva hao kuhakikisha wanajikamilisha kwa vitu vyote vinavyohitajika kama sheria za usalama barabarani zinavyolelekeza ili kuepukana na adha ya kukamatwa mara kwa mara na askari na kutozwa faini

Mh Mariro amesema ni kweli madereva wengi hawajui sheria za usalama barabarani lakini sheria hazitambui kuwa hawafahamu sheria, hivyo ili kuepukana na adha hiyo wanatakiwa kuwa na vitu vyote vinavyohitajika kama leseni ya udereva, leseni ya biashara, bima, kadi ya pikipiki, stika ya nenda kwa usalama, kofia ngumu(helment 2) pamoja na pikipiki yenye vyake vifaa vyote

Amesema kwa kulitambua hilo mkuu huyo atafanya mazungumzo na chuo cha VETA Makete kifanye mafunzo maalum kwa madereva hao kwa gharama nafuu ili wazifahamu sheria za usalama barabarani pamoja na kupata leseni za udereva

Katika kikao hicho madereva hao walikuwa wakiuliza maswali mengi ya ufahamu ambapo walijibiwa maswali yao yote na kuondoka kwa furaha na uelewa wa mambo mbalimbali ya usalama barabarani

Aamka asubuhi na kukuta miguu imekatika

  Mmkazi wa Ludewa, Mkoani Njombe
Mmkazi wa Ludewa, Mkoani Njombe, Yohana Nkwera (54) anadai kukatika miguu katika hali ya kushangaza.
Yohana anasema katika maisha yake amekuwa ni mwenye hofu kubwa baada ya kukumbwa na tukio hilo la aina yake la kukatika miguu akiwa usingizini. Anasema hadi sasa haelewi namna hasa tukio hilo lilivyomtokea, kwani hakuhisi maumivu yoyote .
Anasema tukio hilo la aina yake lilimtokea mwaka 1992, lakini halikuwahi kuandikwa wala kutangazwa, badala yake ni watu wachache waliokuwa wakilifahamu.
Anasema siku hiyo usiku alikwenda kulala kama ilivyo kawaida, alipoamka asubuhi alikuta miguu yake imekatika.
Kilichomshangaza zaidi ni kwamba hapakuwa na damu wala jeraha lilionekana. Palionekana pana kovu, kana kwamba alikatika mguu muda mrefu uliopita.
Anasema mara ya kwanza ulianza kupotea mguu wa kulia, hiyo ilikuwa ni mwezi Machi, 1992. Kutokana na tukio hilo, ndugu zangu walifanya jitihada mbalimbali ikiwemo kufanya maombi katika nyumba mbalimbali za ibada, huku wengine wakienda kwa kuwaona waganga wa jadi.
“Kama binadamu wa kawaida ilichukua muda sana kuamini kilichotokea ndani ya maisha yangu na mguu wangu,” anasema.
Mwezi mmoja baadaye yaani mwezi Aprili mguu wa kushoto nao ulikatika katika mazingira yaliyo sawa na yale ya awali.Inaweza kuwa vigumu kuamini lakini ulimwengu ndivyo ulivyo.
Anakumbuka mazingira ya kukatika kwake yanahusishwa na imani za kishirikina kwa sababu siku chache zilizopita kabla ya kukumbana na dhahama hiyo aliwahi kukorofisha na mtu katika vilabu vya pombe za kienyeji anayesadikiwa kufanya tendo hilo.
Baada ya miaka saba kupita Yohana alipelekwa Hospitali Teule ya Ikonda wilayani Makete kupata huduma za tatizo lake. Alifanikiwa kupata msaada wa baiskeli ya magurudumu, ambayo aliitumia kwa miaka mitano.
Kwa sasa baiskeli hiyo haifanyi kazi kutokana na watu wanaosadikiwa kuwa ni wezi kuiba matairi na vyombo muhimu vinavyoiwezesha baiskeli hiyo kufanya kazi.
Pamoja na kupewa baiskeli hiyo na wasamaria wema, Yohana anakiri pia kuchongewa viatu na hospitali hiyo ambavyo vinamuwezesha angalau kutembea umbali mfupi.
Kutokana na ulemavu huu wa kimiujiza, Yohana anakiri ndoto zake za maisha hazijatimia mpaka leo na inawezekana zikawa zimepotea kabisa.
Mipango yake
Alipinga mambo mengi yakiwemo kusoma na hata kufungua miradi ya maendeleo. Sasa ni kama anaona haiwezekani tena kwa sababu hana uwezo thabiti wa kufanya kazi; ukizingatia ni kijijini ambako kazi kubwa inayotegemewa kiuchumi ni kilimo cha jembe la mkono.
Ulemavu huo umesababisha ashindwe kuoa, kwani anasema katika ulimwengu wa sasa ni ngumu kuoana na mtu kama huna uwezo wa kumhudumia.
Anasema ilikuwa ni ngumu kwa ndugu kuamini kinachotokea lakini anawashukuru wasamaria wema walioendelea kumhudumia mpaka pale alipoikubali hali yake na kuanza kuishi katika huo mfumo mpya wa maisha.
Kwa sasa Yohana anaishi na dada yake mkubwa aitwaye Lucy Nkwera akimsaidia kwa mahitaji ya kila siku ikiwemo chakula na huduma za usafi na usalama kwa jumla.
Akisimulia kwa hisia, Yohana anakumbuka jinsi alivyokuwa katika hali ya uzima wa miguu na kujitegemea, kwamba anashangaa sana kuona leo amekuwa ni mtu wa kuomba msaada; kwa sasa msaada wake mkubwa ni dada yake huyo.
Lucy anasema, “Maisha ni magumu sana kwa kuwa anatakiwa kuwa karibu naye, kwani hakuna mwingine wa kumsaidia.”
Mbali na kupata huo ulemavu wa miguu, Yohana anaumwa ugonjwa wa kifafa, ambao nao aliupata baada ya kukatika miguu.
Ugonjwa huu unamfanya kupoteza fahamu mara kwa mara kitendo ambacho ni hatari kwa afya na maisha yake.
Anamshukuru Lucy kwa kuendelea kumhudumia kwa sababu kwa mazingira ya kawaida ni wachache wenye moyo wa huruma kiasi hicho, hasa kumhudumia mgonjwa ambaye hatarajii kupona leo hata kesho.
Anashukuru pia ndugu zake kutoka maeneo mengine akisema kuwa nao wamekuwa wakija kumtaka hali na kumletea vyakula.
Anaishukuru Serikali ya Kijiji cha Ludewa anachoishi, kwa kumkumbuka na kumhudumia kwa kadiri wanavyoweza.
Anasema kama Serikali na ndugu wasingekuwa wanamsaidia, huenda hali yake ingekuwa ngumu zaidi na ilivyo sasa kwani kwa jumla afya yake ni dhaifu.
Ushauri wake
Yohana anawaomba watu kuachana na tabia za kunyanyapaa walemavu.Anasema baada ya kuwa na ulemavu, kuna marafiki zake walimtenga.
“Inauma sana kuona kumbe wengine ni marafiki wa wakati wa raha...Ukiwa na matatizo wanakukimbia, hii tabia si nzuri, ni lazima tuwe na moyo wa kusaidiana wakati wote,” anasema Yohana.
Anaongeza kuwa hata yeye hakupenda kuwa katika hali ambayo anayo sasa. Ndiyo kusema kwamba yeyote anaweza kupatwa na lolote kabla ya hajafa, tusinyanyasane.
Chanzo;Mwananchi

CCM wawapiga CHADEMA

  • Mbunge CCM aongoza mashambulizi
Green Guard wa CCM wawapiga CHADEMA
KIKOSI cha ulinzi cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Njombe, mkoani Iringa kimewashushia kipigo wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kumvunja taya mwanachama, Ally Kalonga.
Licha ya kushusha kipigo hicho, Mkuu wa Polisi wilayani Njombe, Lucy Mwakafirwa, amelaumiwa kuwakumbatia watuhumiwa makada wa CCM, huku akiwasweka ndani wanachama wa CHADEMA.
Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu kutoka eneo la tukio, mwananchi ambaye hakupenda jina lake litajwe, alisema kikosi cha CCM cha ‘Green Guards’ kilitoa kipigo kwa wafuasi wa CHADEMA baada ya kubaini mpango wao wa kutaka kugawa fedha kwa wapiga kura utabainika.
CCM na CHADEMA wako katika kampeni za udiwani wa Kata ya Njombe Mjini unaotarajiwa kufanyika Februari 9,  sambamba na kata nyingine 27 nchini kote.
“Siku ya leo (jana) tulikuwa na mikutano ya kampeni za udiwani wa Kata ya Njombe Mjini, mikutano ilifanyika salama huku vyama vyote vikimaliza salama,” alisema.
Kwa mujibu wa shuhuda huyo, baada ya kukamilika kwa kampeni hizo viongozi wa CCM wilayani hapo wakiongozwa na mbunge wa chama hicho (jina linahifadhiwa), walielekea katika Kijiji cha Matalawe.
Mwananchi huyo alisema baada ya kufika Matalawe, walikusanya baadhi ya wananchi na kuwaweka katika chumba kimoja na kuanza kugawa fedha.
“Baadhi ya Wana CHADEMA waliokuwepo pale, hawakupendezwa na jambo hilo, hivyo waliamua kupiga simu kwa viongozi wao kuwajulisha mchezo huo mchafu na viongozi hao walichukua gari kuja eneo hilo,” alisema.
Alisema kabla ya kufika walikutana na  kundi la vijana wa CCM waliokuwa wametanda barabarani.
Alisema vijana hao wa CCM waliwaamuru Wana CHADEMA hao wasimame, kisha walichomoa funguo za gari lao lililokuwa likiendeshwa na Ally Muhagama.
“Green Guards walisimamisha gari  la vijana wa CHADEMA, wakamnyang’anya funguo dereva, wakamshusha chini na kuanza kumpiga. Wakati wakiendelea kumpiga, ghafla alitokea mtu mmoja aliyevaa kiraia na kujitambulisha kuwa askari na kuomba wamuachie mtu huyo.
“Kutokana na kauli hiyo mbunge aliyekuwa na vijana wa CCM alimuomba raia huyo  atoe kitambulisho lakini hakuwa nacho, ndipo naye alipogeuziwa kibao na kuanza kupigwa na baadaye walifungiwa kwenye ofisi ya CCM ya eneo hilo,” alisema mtoa habari wetu.
Alisema vijana wa CHADEMA waliojificha baada ya kuona wenzao wakipata kipigo hicho walijaribu kukimbia lakini Green Guards waliwakamata na kuwapa kipigo huku mmoja wao akivunjwa taya na hali yake si nzuri.
“Hata hivyo wananchi walilazimika kupiga simu polisi ambapo walifika na kuwaamuru Wana CCM hao na mbunge wao wawatoe na kuelekea kituo cha polisi,” alisema.
Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, wakiwa polisi, mbunge huyo na viongozi wa wilaya walifika kituoni na kwenda moja kwa moja katika ofisi ya OCD Mwakafirwa.
Mwananchi huyo alisema baada ya dakika chache ilitolewa amri ya kuwasweka ndani wanachama hao wa CHADEMA walioumizwa, huku baadhi yao wakiendelea kuvuja damu.
Gazeti hili lililazimika kumtafuta Mwakafirwa ambaye hakukubali wala kukataa kuwepo kwa vurugu hizo huku akimtaka mwandishi wa habari hizi kuwasiliana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Kamishna Msaidizi (ACP) Ramadhan Mungi, kwa taarifa zaidi.
Kwa upande wake Kamanda Mungi alisema hajapata taarifa kamili na kwamba anafuatilia kujua ukweli na undani wa tukio hilo
Chamzo:Tanzania Daima 
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa