DK. MAHANGA ATEMBELEA VIWANDA, MASHAMBA YA CHAI NJOMBE


Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,  Dk. Makongoro Mahanga (kulia) akioneshwa mitambo ya kuzalisha majani ya chai katika Kiwanda cha Chai cha Luponde, wilayani Njombe, alipofanya ziara ya kutembelea viwanda na mashamba ya chai  pamoja na kuzungumza na wafanyakazi. Kushoto ni Meneja wa Uzalishaji wa kiwanda hicho, Antony Mwai.
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,  Dk. Makongoro Mahanga akionja aina jibini (cheese) zinazozalishwa na Kiwanda cha Maziwa  cha CEFA Njombe, wilayani Njombe, alipotembelea kiwanda hicho hivi karibuni.
 Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk. Makongoro Mahanga (kushoto) akizungumza na Meneja Biashara wa Kiwanda cha Chai Luponde, Athanas Mwasamene alipotembelea hivi karibuni  shamba la majani ya chai-dawa (herbal tea) wilayani Njombe. Dk. Mahanga alifanya ziara wilayani humo ambapo alitembelea viwanda, mashamba ya chai pamoja na kuzungumza na wafanyakazi.
 Meneja Uzalishaji wa Kiwanda cha Chai Luponde, wilayani Njombe,  Anthony Mwai (mbele) akimwonesha Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk. Makongoro Mahanga (katikati), shehena za chai-dawa (herbal tea) zinazozalishwa kiwandani hapo, tayari kusafirishwa kuuzwa nje ya nchi. Dk. Mahanga alifanya ziara wilayani humo ambapo alitembelea viwanda, mashamba ya chai pamoja na kuzungmza na wafanyakazi.

CHANZO: MICHUZI BLOG

MKUU WA WILAYA YA MAKETE AWATAKA NLC KUMALIZA TOFAUTI NA KKKT KATIKA WILAYA HIYO.




NA James Festo, Makete

Mkuu wa wilaya ya makete bi. Josephine matilo amewataka viongozi wa dhehebu la kanisa la kiinjili la kilutheli KKKT Dayosisi ya kusini kati kumaliza tofauti zilizopo baina yao na viongozi wa huduma ya maisha mapya ndani ya kristo NLC wilayani hapa.


Ameyasema hayo akiwa mgeni rasmi wakati wa kufungua mkutano wakuelekea kilele  maadhimisho ya miaka hamsini ya huduma hiyo ya maisha mapya ndani ya kristo ambao utadumu kwa siku saba ambao unafanyika  katika viwanja vya mabehewani kijiji cha iwawa  na kuwataka kudumisha amani na mshikamano ili kuweza kuyafikia malengo yao.


'viongozi tunakaa tunarumbana tunawapotosha wananchi tukae meza moja ili kuweza kumaliza tofauti zetu na si kuendelea kila watu kivyao hapo mnawaumiza  wananchi sote mungu wetu ni mmoja malumbano  yanatoka wapi?' aliuliza bi matilo.


Aidha mgeni rasmi huyo bi matilo ameeleza kuitambua huduma hiyo na kuwashauri viongozi na kuwataka kueneza dini jinsi katiba yao inavyosema  bila ya kuvunja katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania


sisi kama serikali tunatambua huduma yenu na tunataka injili ifike kila mahala  kwa jinsi mlivyoyaainisha malengo yenu ya kuweza kuimarisha amani na utulivu kwa wananchi na hatutakaa kimya kama kuna kanisa linapotosha wananchi  alisema bi matilo.


kwa Upande wake katibu mkuu taifa  wa huduma hiyo bw. Daimon Mwandambo wakati akisoma risala kwa mgeni rasmi alisema kwa huduma hiyo imesambazwa katika mikoa 18 ya tanzania bara na kuufanannisha utofauti huo na uliowahi kujitokeza jijini dar es salaam na ule wa mkoani iringa ambao ulidumu kwa miaka saba.  

CHANZO: JIACHIE BLOG
Mkutano huo utakaodumu kwa siku saba ambapo kilele cha maadhimisho hayo yatakuwa septemba 13 na mkutano mkuu kitaifa utafanyika mkoani morogoro pia katika ufunguzi huo  ulilhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa huduma hiyo  wakiwemo uongozi wa mkoa serikali akiwemo mwenyekiti wa halmashauri bw daniel Okoka na mwakilishi wa mkurugenzi bw. jakob mena, viongozi siasa nawageni wengine waalikwa.  

MWANAFUNZI ALAZIMISHWA NGONO BILA KONDOMU NA MAJANGA MENGINE WILAYANI MAKETE

Kata ya Iwawa ilipo shule hiyo.
 
Na Edwin Moshi wa Globu ya Jamii, Makete
Wafunzi wa shule ya sekondari Iwawa wilayani Makete mkoani Njombe wamekiri uwepo wa wanafunzi wenzao ambao wanajihusisha na vitendo vya ngono na wengine wanaishi na virusi vya UKIMWI, licha ya jamii kudhani kuwa wanafunzi hawawezi kuwa na virusi hivyo kwa minajili kwamba bado ni wadogo.
Hayo yamebainika baada ya mtandao huu kufanya mahojiano ya kina na baadhi ya wanafunzi wanaosoma shuleni hivi karibuni kwa ruhusa ya mkuu wa shule hiyo Bw. Christopher Haule hapo kufuatia wananchi wengi wilayani hapo kudhani kuwa wanafunzi hao hawana maambukizi ya vvu kwa kuwa ni wadogo na huwenda hawajaanza kujihusisha na vitendo vya ngono. Mwanafunzi mmoja (jina linahifadhiwa kwa sababu za kimaadili) amesema ana marafiki zake zaidi ya watano ambao wanaishi na virusi vya UKIMWI na hajui walivipataje, hivyo anaamini wapo wanafunzi wengi ambao wana maambukizi.
Amesema jamii inapaswa kuondokana na dhana potofu kuwa mabinti ama vijana wadogo hawana vvu waache mara moja kwa kuwa virusi vinampata mtu yeyote bila kujali umri.
“Mtu anayedhani kuwa wanafunzi huwa hawana vvu ni uongo, na pia waanatakiwa kuacha kujihusisha kimapenzi na wanafunzi kwa madai kuwa hawana vvu, lakini wakumbuke sheria za nchi haziruhusu kujihusisha kimapenzi na wanafunzi, jamani Ukimwi upo kwa kila mtu” alisema mwanafunzi huyo. Mwanafunzi mwingine amesema yeye hafahamu kama wanafunzi hao wenye vvu wanajihusisha kimapenzi na watu kwa kuwa wapo ambao wanaishi na wazazi wao na wengine wamepanga kwenye nyumba maarufu kama mageto ambao kwa kiasi kikubwa wako huru kufanya mambo yao kwa kuwa hawana muangalizi. “Ni kweli kabisa wapo wanafunzi wenye vvu wanaoishi wenyewe kwenye mageto, lakini mimi sijui kama wana wapenzi ama lah, maana ni ngumu kujua na mimi sipo hapa kwa ajili ya kufuatilia maisha ya mtu, na hao ninao kwambia kwa kuwa ni marafiki zangu na waliwahi kuniambia kuwa wanaishi na vvu” alisema mwanafunzi huyo(jina tunalo)

Mmoja wa mwanafunzi aliyezungumza na mtandao huu
 
Mwanafunzi upande wa kushoto wa picha hii amemweleza mwandishi wetu kuwa mpenzi wake anamlazimisha kufanya mapenzi bila kondomu
 
“Mimi kwa upande wangu Kusema kweli nina mpenzi na nilishawahi kupima vvu mwaka jana (2012) na kujikuta sina maambukizi namshukuru Mungu kwa hilo, na pia nimekuwa nikifanya mapenzi kwa kutumia kondomu lakini kuna wakati mwingine hatutumii mimi na mpenzi wangu na mara nyingi yeye ndiyo ananishawishi tusitumie, na huyo mpenzi wangu si mwanafunzi ni jamaa tu wa pale mtaani kwetu, na mimi huwa nakwenda home kwake(Nyambani kwake) na wakati mwingine anakuja geto kwangu, ili atumie kondom huwa namwambia leo ni siku zangu za hatari, hapo ndipo atavaa kondomu” alisema mwanafunzi huyo wa kike ambaye anaishi kwenye nyumba ya kupanga. Akizungumzia suala hilo, diwani wa kata ya Iwawa Benjamin Mahenge alikiri kuwepo kwa tatizo la ukimwi kwa kila mtu, na kuongeza kuwa hata wanafunzi wapo wenye vvu ingawa ni kwa kiasi kidogo ukilinganisha na miaka iliyopita na pia wapo wanafunzi wanaojihusisha na vitendo vya ngono, na ambao wameshabainika wamefikishwa kwenye vyombo vya sheria
Diwani wa kata ya Iwawa Benjamin Mahenge (kushoto) akizungumza na mwandishi wa habari hizi
"Unajua ni ngumu mwanafunzi kuniambia mimi ama kiongozi mwingine kuwa anajihusisha kimapenzi na mtu lakini kwako mwandishi kasema, mimi ninaomba wawe wawazi ili tuweze kuwasaidia hasa pale linapojitokeza tatizo hasa mimba kwa kuwa hawawataji wahusika" alisema Mahenge
Mahenge amesema huu ni muda wa jamii kubadilika na kuondokana na dhana potofu kuwa wanafunzi hawawezi kuwa na vvu, na pia wawaache wanafunzi hao wasome na si kuwarubuni na kujikuta wakifanya nao mapenzi Pia amesema wapo wanafunzi katika kata yake ambao wamepanga na uangalizi wao si mzuri kwa kuwa wanajiamulia mambo yao wenyewe hata kama si mazuri kutokana na kukosa uangalizi wa watu wazima.
 “Unakuta mwanafunzi kajipangia kwenye chumba chake, yeye ndio kila kitu, akitaka kusoma haya, akitaka kwenda disco hakuna wa kumuuliza, hii ni hatari pia” alisema Mahenge
 
 Moja ya nyumba iliyoko Makete mjini amayo wanafunzi wamepanga
 
Kwa Hisani ya Edwin Moshi

MKUU WA WILAYA WA MAKETE ATAKA ELIMU YA VVU IENDE PAMOJA NA UJASILIAMALI


 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mradi huo ngazi ya wilaya akisikiliza maelezo ya mradi huo kutoka SUMASESU
 Mkurugenzi wa shirika la SUMASESU Egnatio Mtawa akitoa maelezo kwa washiriki kuhusu utambulisho wa mradi uitwao "Vijana wa makete na mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi" katika ukumbi wa HIMA Makete wakati wa utambulisho wa mradi huo ngazi ya wilaya Augusti 09, 2013. Shirika la SUMASESU ndilo litakalotekeleza mradi huo kwa ushirikiano na UNICEF
 Washiriki wakisikiliza maelekezo kutoka kwa mkurugenzi wa SUMASESU (hayupo pichani)
 Mratibu wa ukimwi halmashauri ya wilaya ya Makete CHAC Ester Lamosai(kushoto) akiwa na Anifa Mwakitalima kutoka SUMASESU
Mtaribu wa ukimwi sekta ya afya (DAC) Dk Shadrack Sanga akichangia hoja kwenye kikao hicho
 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mradi huo ngazi ya wilaya katika ukumbi wa HIMA Makete
Makamu mwenyekiti halmashauri ya wilaya ya Makete Jison Mbalizi akiahirisha kikao hicho
***********************888888
Na Edwin Moshi, Makete 

Wadau wa mapambano dhidi ya virusi vya Ukimwi kwa vijana wilayani Makete mkoani Njombe wametakiwa kutoa elimu hiyo sanjari na elimu ya ujasiriamali kwa pamoja kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kupunguza ongezeko la maambukizi ya ugonjwa huo kwa kasi zaidi

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro wakati akifungua mradi wa vijana wa Makete na mapambano dhidi ya UKIMWI uliozinduliwa Ijumaa Agosti 9, 2013 ngazi ya wilaya, mradi ambao utatekelezwa na shirika la sumasesu kwa ufadhili wa UNICEF

Matiro amesema vijana wengi wamekuwa wakipatiwa elimu hiyo ya namna ya kujilinda na maambukizi mapya ya vvu na baada ya hapo wanakosa kazi ya kufanya hivyo kuwa rahisi kwao kujiingiza kwenye vitendo vitakavyowasababishia kupata vvu

"Kijana anapewa elimu sawa lakini hana cha kufanya mwishowe akija mtu wa kuwarubuni hasa kifedha wanaingia kilaini kwa kuwa hana shughuli yeyote inayomuingizia kipato, mwishowe anaweza kupata vvu"alisema Matiro

Amewataka vijana kujiunga na vikundi mbalimbali ili waweze kupatiwa mikopo nafuu kwa ajili ya shughuli hasa kilimo kwa kuwa wakishajiunda na kutoa taarifa yeye kwa kushirikiana na halmashauri watawasaidia kupata mkopo ambapo wakati huo huo wakiwa na shughuli ya kufanya halafu wakapata elimu ya kujikinga na vvu itakuwa bora na yenye manufaa kwao

Wadau walioshiriki katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa HIMA Makete akiwemo mratibu wa ukimwi sekta ya afya (DAC) Dk Shadrack Sanga amelitaka shirika hilo wakati wa kutekeleza mradi huo watoe elimu ya tohara kwa vijana wa kiume ambapo akiwataarifu wao kama idara ya afya wako tayari kuungana nao jambo lililoungwa mkono na kaimu mganga mkuu Boniphace Sanga ambaye alikuwepo kwenye kikao hicho

Kwa upande wao shirika la SUMASESU kupitia kwa mkurugenzi Egnatio Mtawa alipongeza kwa ushirikiano uliooneshwa na wadau wote huku akimuahidi mkuu wa wilaya kuwa wataingiza mada ya ujasiriamali wakati wakitoa elimu ya ukimwi kwa vijana ili iwasaidie huku akiahidi kushirikiana na kila wahusika ili mradi huo ufanikiwe

Mradi huo utakaotekelezwa hadi Julai 2015, utahusisha kata za Ipelele, Iniho, Iwawa, Isapulano na Kitulo
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa