Mwanafunzi ajinyonga Njombe

WATU watatu wamekufa mkoani Njombe katika matukio tofauti likiwemo la ajali iliyosababisha mwanafunzi kupoteza maisha  na wengine wawili kujinyonga.

Kamanda wa polisi mkoani Njombe kamishna msaidizi wa polisi Fulgence Nginyani amesema katika tukio la kwanza, la april 19 saa 11 jioni katika maeneo ya uwanja wa polisi makambako, mwanafunzi aliyetambuliwa kwa jina la jina la Helen Mwitula (9) mwanafunzi wa shule ya msingi Mwembetogwa  darasa la tatu alikufa baada ya kugongwa na gari.

Kamanda Ngonyani amesema,ajali hiyo ilisababishwa na gari lenye namba T. 809 BHC double Cabin pick-up mali ya kampuni ya Jah- People investment  Ltd. ya mjini makambako lililokuwa likiendeshwa na dereva Seily Mtafya (28) ambapo katika ajali hiyo hiyo,mwanafunzi mwingine Joyce mwakipesile (9) amelazwa katika hospitali ya kkkt ilembula baada ya kuvunjika miguu yote miwili.

Katika tukio jingine april 19 Oktar Mahenge (12) mwanafunzi wa darasa la na tano katika shule ya Lupalilo wilayani Makete alijinyonga hadi kufa kwa kutumia koti la suti nje ya nyumba yao.

Wakati huo huo, Ezekiel Haule (28) mkazi wa kijiji cha Kiwe kata ya Mawengi wilayani Ludewa alikutwa akiwa amekufa baada ya kujinyinga na kamba ya manila porini nje ya nyumba yake chanzo kinachunguza.

Afariki kwa kupigwa na kuvunjwa viungo vya mwili

MTU mmoja mwanaume amekufa wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Kibena mkoani Njombe, baada ya kukutwa akiwa amepigwa na watu wasio julikana mjini Makambako.

Kamanda wa polisi,kamishna wa polisi mkoani humo, Fulgence Ngonyani, amemtaja mtu huyo kuwa ni Peles Sanga (33) mkazi wa mji mwema makambako ambaye Aprili 10 saa 10 alfajiri alipokutwa katika pipeline akiwa amevunjwa miguu yote miwili, na mkono wa kulia kisha kutelekezwa eneo la tukio.

Kamanda Ngonyani amesema, mtu huyo aliokotwa na wasamalia kisha kufikishwa katika kituo cha afya ambapo alihojiwa na kueleza bayana kuwa alitoka matembezini na kuvamiwa na watu watatu ambao walivalia makoti meusi marefu,ambao baada ya kumjeruhi walitokomea kusiko julikana.

Marehemu alifikishwa kibena na kuanza matibabu ambapo hata hivyo alikufa saa 6 mchana april 11, baada ya  kuvuja damu nyingi katika majeraha, na jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa