Home » » Pinda ahimiza kilimo cha mazao ya biashara Njombe

Pinda ahimiza kilimo cha mazao ya biashara Njombe

WANANCHI wilayani makete Mkoani Njombe, wametakiwa kuboresha mazao ya biashara ambayo yanastawi katika Wilaya hiyo,ili kukuza uchumi kupitia rasiliamali walizo nazo.

Akizungumza na wananchi waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda ameagiza wananchi kuimarisha mazao ambayo ni muhimili wa uchumi wao.

Amewaondoa shaka wakulima hao kuhusu wanunuzi wa zao la Pareto na kuongeza kuwa kilimo cha matunda, Pareto vinapaswa kuboreshwa ili kuutumia vema fursa ya kilimo katika uzalishaji mazao yanakubalika kimataifa.


Kambarage Sanga ni mkulima wa matunda  anayemiliki ekari 3000 za matunda, katika kijiji cha Iniho, akamweleza waziri mkuu jinsi anavyoendesha kilimo cha matunda aina mbalimbali.

Baada ya kutembelea bustani ya miche ya matunda na kujionea shughuli za uzalishaji zianazofanywa na wanakikundi wa kilimo cha matunda KIWAMAI ameahidi kuwapa mashine ya kukamilia juisi ya matunda yenye thmanai ya sh. milioni 5.2.

Afisa kilimo wa wilaya hiyo, akisoma tarifa ya kilimo cha matunda mradi ambao unahudumiwa na halmashauri hiyo, huku wanakikundi wa KIWAMAI wakaeleza changamoto ambayo ni kikwazo cha malengo waliyokusudia

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa