Home » » Njombe wavalia njuga usafi wa mazingira

Njombe wavalia njuga usafi wa mazingira



ASASI zizizokuwa za kiserikali zimeendelea kujadili utekelezaji wa  mpango wa kuboresha usafi wa mazingira shuleni,  kupitia mradi wa  TAWASANET  wa uboreshaji wa huduma za  maji na usafi wa mazingira shuleni ambao umefadhiriwa na shirika la kuhudumia watoto Duniani UNICEF.

Mpango huo ambao umeanza mapema mwaka huu, umehusisha wadau kutoka asasi za kiraia ambazo zimeshiriki katika kujadilli suala la usafi shuleni mradi ambao umetolewa na SWASH  asasi inayojihusisha na huduma za afya ya maji na usafi wa mazingira,  ambapo awali mafunzo yalitolewa kwa wadau wa mazingira ili kuwajengea uwezo wa kusimamia usafi wa mazingira,Mkoani Njombe na kuanza kwa shule  mbili za majaribio .

UNICEF kwa kushirikianana SNV shirika la Kiholanzi, wameelekeza jitihada za usafi wa mazingira shuleni katika Wilaya ya Njombe na kufanikisha kuzifikia shule tano ambazo zimeanza kwa majaribio.

Katika jitihada za kuhakikisha usafi wa mazingira shuleni unazingatiwa, baada ya kufanya majaribio la utoaji elimu kwa wadau hao, mabadiliko yameonesha kuanza kuchomoza katika shule ambazo mpango umeanza kutekelezwa, Dkt Rosmary Daniel ni mratibu wa TAWASANET anaeleza kuhusu mradi huo.
Insert Dkt. Rosemary Daniel mratibu TAWASANET. 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa