Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda apokea mitambo ya kisasa ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akipokea mfano wa Ufunguo kutoka kwa Mkurugenzi wa kamapuni ya GF Trucks & Equipment Ltd ya jijini Dar es Dar es Salam Bw. Imran Karmali baada ya makabidhiano ya Mitambo ya Kisasa ya kutengeneza Barabara na miundombinu kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe. Mitambo hiyo imenunuliwa kwa gharama ya Tsh. Million 700 kwa makubaliano maalum ya mkopo nafuu usiokuwa na riba. Kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd Mehboob Karmali na aliye kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Njombe George Mkindo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akijaribu mojawapo ya mitambo hiyo mara baada ya kukabidhiwa rasmi kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe. Pembeni yake ni Mkurugenzi wa kamapuni ya uuzaji mitambo hiyo ya Jijini Dar es Salaam ya GF Trucks & Equipment Ltd Bw. Imran Karmali.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akifurahia mojawapo ya mitambo ya kisasa ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine iliyonunuliwa na Halmashauri ya Mji wa Njombe kutoka Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd. Pembeni yake ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Imran Karmali, Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Bw. Mehboob Karmali na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Njombe George Mkindo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimkabidhi mfano wa Ufunguo wa Mitambo hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Mji wa Njombe George Mkindo mara baada ya kuipokea kutoka kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd ambayo ndio walioiuzia Halmashauri hiyo mitambo hiyo.
Spika wa Bunge akitoa shukrani zake kwa uongozi wa Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd kwa kuiwezesha Halmashauri ya Mji wa Njombe kupata Mitambo ya kisasa ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine iliyonunuliwa na Halmashauri ya Mji huo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimsikiliza kwa makini Afisa Mauzo Mwandamizi wa kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd Mhandisi Juma Hamsini alipokuwa akielezea ubora wa mitambo ya kampuni hiyo kabla ya kumkabidhi rasmi Mhe. Spika kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe. Mitambo hiyo imenunuliwa kwa gharama ya zaidi ya Milion 700 za Kitanzania kwa makubaliano ya mkopo usiokuwa na riba kutoka Mfuko wa Halmashauri ya Mji wa Njombe. Kulia kwa Mhe. Spika ni Mwenyekiti wa Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd Mehboob Karmali na walioko kushoto ni watendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo wakiongozwa na George Mkindo (mwenye koti)Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Njombe George Mkindo akitoa pongezi zake kwa kampuni ya uuzaji wa mitambo ya ujenzi ya GF Trucks & Equipment Ltd baada ya kukubali kuizia Halmashauri yake Mitambo ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine katika Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa Mkopo usio kuwa na Riba wa kiasi cha Million 700 za Kitanzania.
Mhe. Makinda akifanya mahojiano na waandishi wa habari mara baada ya kupokea mitambo hiyo.
Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge.

SEMINA YA SIKU YA MAWASILIANO NA HABARI JAMII DUNIANI YAFANA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MANYUNYU MKOANI NJOMBE

 Viongozi wa TCRA ,Walimu na wanafunzi wakielekea ukumbini katika sherehe hizo 

Wadau Mbali mbali wakisikiliza wakati Semina hiyo inaendelea jana
Kaimu Meneja wa mawasiliano Kanda Ndugu Asajile akiwafundisha wanafunzi umuhimu wa vifaa mbali mbali vya Digital
 Wanafunzi wa Shule ya Manyunyu Mkoani Njombe wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi 

 Wanafunzi wa Shule ya Manyunyu Mkoani Njombe wakionesha vipaji vyao katika sherehe hizo 


 Shule ya Sekondari ya wasichana Manyunyu wakikabidhiwa Tv ya kisasa yenye inch 32 LCD


Baadhi ya zawadi walizo kabithiwa shule ya wasichana ya Manyunyu Mkoani Njombe 

Mgeni Rasmi akimkabidhi zawadi mwanafunzi aliye jibu maswali vizuri Hidaya Mapunda aliyepata Laptop ya kisasa 

 Mwanafunzi Hidaya Mapunda akiwaonesha wenzake Laptop yake 
 Mgeni Rasmi katika Sherehe hizo akiendelea kukabidhi zawadi mbali mbali Shuleni hapo 
 Wanafunzi walio Hudhuria katika Sherehe hizo za Siku ya mawasiliano 
 Mgeni Rasmi akipanda Mti shuleni hapo mara baada ya kumaliza shughuli zote 

Habari kamili itawajia siku ya Sherehe zenyewe 
Picha zote na Joseph Mwaisango wa Mbeya yetu Blog





WASICHANA WA SHULE YA SEKONDARI MANYUNYU NJOMBE WAFAIDIKA NA SEMINA YA KUTUMIA KOPYUTA NA UMUHIMU WA MFUMO WA DIGITAL

Wasichana wa shule ya sekondari ya wasichana manyunyu mkoani njombe wakimsikiliza mwana sayansi wa masafa
Peter Kihogo kutoka mamlaka ya mawasiliano kanda ya nyanda za juu kusini

Mwanasayansi wa masafa Peter Kihogo akiendelea kuwaelimisha wasichana wa shule ya sekondari manyunyu juu ya umuhimu wa mawasiliano na faida zake katika masomo na shughuli mbalimbali za kila siku katika jamii

Katibu muhtasi mamlaka ya mawasiliano kanda ya nyanda za juu kusini Frida Msese akipeana ushauri na wasichana wa shule ya sekondari manyunyu

Wanafuzi wakiwa makini kumsikiliza mwanasayansi wa masafa


Mkuu wa shule ya ya sekondari manyunyu  Adolphina Katembo akiwashukuru waedesha semina ya mawasiliano na habari jamii toka mamalaka ya mawasiliano kanda ya nyada za juu kusini kuichagua shule yao kuwa mojawapo ya shule katika kupewa semina hiyo ya mawasiliano duniani

MWANAMKE ASWAKWA KWA KUTOROSHA MTOTO NA FEDHA TSH.MILIONI 15 MAKAMBAKO NJOMBE

Mwanamke Queen Daniel Chonya (26) anayedaiwa kumtorosha mtoto na kukimbia na kiasi cha shilingi milioni 15 za mumewe






Mtoto anayedaiwa kutoroshwa




Mwanamke mkazi wa mji wa Makambako wilaya ya Njombe mkoa wa Njombe Queen Daniel Chonya (pichana juu) anatafutwa na mume wake mfanyabiashara wa mji wa Makambako Timoth Mbuma kwa tuhuma za kumtorosha mtoto pamoja na kukimbia na kiasi cha fedha kiasi cha shilingi milioni 15.


Akizungumza na mtandao huu wa http://www.francisgodwin.blogspot.com/ mfanyabiashara huyo Bw Mbuma amesema kuwa mwanamke huyo ametoroka na mtoto wa kiume mwenye mwaka mmoja na miezi mitano anayeitwa Given au Juniour na kuwa mwanamke huyo mkazi wa Malangali wilaya ya Mufindi ambaye ameishi naye kwa miaka minne sasa katika eneo la Mwembetogwa mji wa Makambako.




Ameongeza kuwa kabla ya kutoweka yeye na mkewe huyo hapa kuwa na ugomvi wowote na kuwa machi 19 siku ya jumatatu asubuhi ambapo alimuita dukani kwa ajili ya kutumwa bank ya NBC kupeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 15 .


Baada ya kupewa fedha hizo alikwenda nyumbani na kufungasha baadhi ya vitu kama nguo na vyombo na kutoweka na kuwa mwanamke huyo anasemekana yupo jijini Mwanza ama jijini D'Salaam na kuwa hadi sasa tukio hilo limeripotiwa polisi kwa kumbukumbu namba MKB/RB/709/12 na kuwa kwa yeyote mwenye taarifa anaweza kutumia namba 0752242464 au 0786505524 ama 0655505524 kuwa kubwa hapa anahitaji mtoto na kuwa mtu yeyote mwenye taarifa sahihi alipo mwanamke huyo atazawadiwa donge nono



 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa