Home » » Karibu Mkoa Mpya wa Njombe

Karibu Mkoa Mpya wa Njombe



Mkoa mpya wa Njombe
Mkoa wa Njombe ni moja kati ya mikoa mipya Tanzania, ukiwa umeanzishwa rasmi mwaka 2012. Umepakana na mikoa ya jirani ya Morogoro, Ruvuma, Mbeya na Iringa.
Mwaka 2002 katika eneo hilo kulikuwa na wakazi 654,929 [1] katika wilaya zifuatazo: Makete (wakazi 106,061), Njombe (wakazi 420,348), Ludewa (wakazi 128,520).
Kutokana na hadhi mpya, wilaya ya Njombe imegawanyika kati ya ile ya mjini na ile ya vijijini. Pia imeanzishwa wilaya ya Wanging'ombe.
Makao makuu yako Njombe mjini.
Wenyeji wa mkoa ni hasa kati ya makabila yafuatayo: Wabena, Wakinga, Wapangwa, Wawanji, Wakisi na Wamanda.



0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa